Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kazi na dawa, taswira Marrakesh, #COP22

Kazi na dawa, taswira Marrakesh, #COP22

Mkutano wa 22 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi COP22 unaendelea huko Marrakesh, Morocco. Mkutano huu unajadili mada tofauti kwa ajili ya kuwezesha jamii na serikali kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi sanjari na kufanikisha kutekeleza mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi uliopitishwa mwaka jana. Kando na mada zikiangazia maswala hayo muhimu, wakazi wa Marrakesh waliandaa tumbuizo, yaani kazi na dawa. Basi ungana na Grace Kaneiya katika makala hii kufahamu walifanya nini.