Neno la wiki- Budi na Mujibu
Katika Neno la Wiki hii Novemba 11 tunaangazia maneno budi na mujibu na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, huko nchini Tanzania.
Bwana Sigalla anasema katika lugha ya kisawhili kuna maneno hayasimami peke yake na ni lazima yaanze na maneno mengine kwa mfano budi lazima lianze na kikanushi kama sina budi nalo mujibu lazima liambatane na ‘kwa’ yaani kwa mujibu wa