Vijana mjini Mogadishu wataka jiji lenye amani
Nchini Somalia, vurugu na ripoti za mapigano kila uchao huweka fikra ya kwamba hakuna maisha ya kawaida nchini humo. Fikra hizo zilizoota mizizi zimefanya vijana wa kisomali hususan kwenye mji mkuu Mogadishu kupaza sauti wakitaka harakati za kuchochea amani na ustawi wa kiuchumi kwa mustakhbali bora wa jiji lao. Vijana hao walipaza sauti zao kwenye kampeni iliyopatia maudhui, ‘Jiji tulitakalo” na Brian Lehander ni shuhuda wetu..