Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Muungano wa kikanda ni muarobaini wa kukuza uchumi Afrika :ECA

Muungano wa kikanda ni muarobaini wa kukuza uchumi Afrika :ECA

Kamisheni ya uchumi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Afrika  ECA kwa kushirikiana na ofisi yake ya jumuiya ya Afrika Mashariki , wameratibu majadiliano ya kisiasa hii leo mjini Kigali Rwanda yenye maudhui ya maendeleo ya Afrika kupitia ushirikiano wa kikanda.

Akizungumza na idhaa hii kandoni mwa mjadala huo,  Balozi wa  Tanzania nchini Rwanda Ali Siwa ameelezea manufaa ya mjadala huo.

( SAUTI BALOZI ALI-1)

Katika mjadala huo Tanzania imetajwa kuwa nchi inayoongoza kwa kunufaika kibiashara miongoni mwa nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki .

( SAUTI BALOZI ALI-2)