UNFPA yaangazia harakati za kumuinua msichana
Ripoti ya hali ya idadi ya watu duniani inazinduliwa leo ambapo shirika la idadi ya watu la Umoja wa Mataifa, UNFPA linasema ripoti hiyo inaangazia
jitihada zinazopigiwa upatu kumuinua mtoto wa kike.
Akihojiwa na Idhaa hii kuhusu ripoti hiyo, Bwana Samwel Msokwa ambaye ni meneja wa mipango UNFPA nchini Tanzania ameisifu kauli ya mbinu ya mwaka huu ya kuangaazia mipango ya kumuendeleza mtoto wa kike ambapo anafafanua yale waliyopatia kipaumbele.
(Sauti ya Msokwa)
“Ni kuelimisha na kumhamasisha....
Amesema UNFPA inaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania na mashirika yasiyo ya serikali ili kuendeleza ajenda ya kumhamasisha msichana kwa njia tofauti na kwamba..
(Sauti ya Msokwa)
“Ndoto ya msichana....