Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kiwanda cha kuzalisha mende na funza kuokoa wafugaji Tanzania

Kiwanda cha kuzalisha mende na funza kuokoa wafugaji Tanzania

Wiki ya vijana imefunga pazia huko nchini Tanzania, tukio ambalo liliandaliwa kwa pamoja na Umoja wa Mataifa na serikali ya Taifa hilo. Wakati wa wiki hiyo iliyofanyika mkoani S  imiyu, Umoja wa Mataifa ulitumia fursa kuchagiza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, hasa ni kwa jinsi gani vijana wanaweza kusongesha ajenda hiyo. Miongoni mwa washiriki alikuwa kijana Riula Daniel ambaye ameonyesha kiu yake ya kukataa umaskini na kutokomeza magonjwa kwa kubuni jinsi ya kuzalisha mende na funza kibiashara. Je anafanya nini? Stella Vuzo, Afisa wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini Tanzania alizungumza naye na Riula alianza kwa kuelezea kile anachofanya...