Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mtu akipatiwa fursa lazima atabadilika - Assaf

Mtu akipatiwa fursa lazima atabadilika - Assaf

Mwimbaji nyota wa kipalestina, Mohamed Assaf ni balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA. Yeye hutumia kipaji chake cha kuimba ili kuinua matumaini miongoni mwa wale ambao hata leo yao ni ndoto, sembuse kesho. Assaf alifika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa tumbuizo maalum na ndipo alipofunguka kuhusu nyimbo zake na nafasi yake katika kuleta nuru kama inavyoelezea makala hii inayoletwa kwako na Assumpta Massoi.