Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi na adha ya kusaka huduma

Wakimbizi na adha ya kusaka huduma

Kuelekea mkutano wa ngazi ya juu kuhusu masuala ya wakimbizi na wahamiaji duniani, utakaofanyika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani, mwandishi wetu nchini Uganda, John Kibego amefuatilia madhila wanayokumbana nayo wakimbizi na wahamiaji nchini humo wakati serikali nayo ikihaha kuwapatia makazi na huduma za kijamii. Mathalani baadhi ya watu wa kabila la jamii la Alur, wenye asili ya Uganda wanaonekana kuwa ni wakongo, na hivyo kukumbwa na madhila wanaposaka huduma. Hayo ni mengine mengi ameyafafanua katika makala hii.