Tangu kifo cha mtoto Alan, maafa bado yaongezeka- UNHCR
Ni mwaka mmoja sasa tangu dunia ishuhudie picha ya Alan Kurdi, mtoto kutoka Syria ambaye alipatwa na mauti wakati boti alimokuwa akisafiria na familia yake kuzama bahari ya Mediteranea wakati wakieleka Ulaya kusaka hifadhi.
Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, huko Geneva, Uswisi, William Spindler amesema inakadiriwa kuwa tangu kifo cha Alan, kuna zaidi ya watu Elfu Nne waliopoteza maisha kwenye bahari ya mediterania, mwaka huu pekee.
Amesema mwaka huu umekuwa wa maafa zaidi katika historia kwenye bahari hiyo akisema…
(Sauti ya Willliam)
“Nafasi ya kupatwa na mauti kutoka Libya kwenda Italia ni mara kumi zaidi ukilinganisha ile ya kuvuka kupitia Uturuki kwenda Ugiriki. Kutokana na maafa haya ya kila kukicha, kuna umuhimu wa nchi husika kufikia mbinu mbadala ikiwa pamoja na hifadhi ya kudumu kwa wakimbizi, wahisani binafsi wajitokeza na pia kunganisha familia zilizotengwa ili kupunguza maafa katika safari hizi hatari baharini.