Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatua za Uganda kwa wakimbizi zamshangaza mkuu wa UNHCR

Hatua za Uganda kwa wakimbizi zamshangaza mkuu wa UNHCR

Sudan Kusini, mzozo ulioanza mwezi Disemba mwaka 2013 umesababisha maelfu ya raia kukimbilia nchi jirani ikiwemo Uganda. Hivi karibuni, Kamishana Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR Filipo Grandi alizuru kambi ya wakimbizi ya muda wa Nyumanzi kaskazini mwa Uganda, lengo la ziara ikiwa ni kutathmini jinsi hali yalivyo kambini humo na jinsi maafisa wa Umoja wa Mataifa wanavyoendesha shughuli yao. Je hali ilikuwaje? ungana basi na Briann Lehander katika makala hii.