Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakazi wa Beni, DRC waandamana kupinga mauaji ya raia.

Wakazi wa Beni, DRC waandamana kupinga mauaji ya raia.

Wiki iliyopita, mamia ya vijana wa kike na wa kiume, waliandamana huko Beni, jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC wakipinga mauaji yaliyofanyika usiku wa kuamkia tarehe 14 Agosti nchini humo.

Umoja wa Mataifa umelaani vikali mauaji hayo yaliyosababisha raia wengine kujeruhiwa. Takwimu zinaonyesha kuwa tangu Oktoba mwaka 2014,zaidi ya raia 700 wameuawa kwenye eneo hilo na tishio ladaiwa ni waasi wa ADF na vikundi vingine vilivyojihami. Wananchi wanapaza sauti kama anavyosimulia Assumpta Massoi kwenye makala hii.