Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Malaria haiongozi tena kwa vifo kwa watoto Afrika- WHO

Malaria haiongozi tena kwa vifo kwa watoto Afrika- WHO

Malaria sio chanzo kikuu tena cha vifo kwa watoto Afrika Kusini mwa jangwa la sahara, Afrika. Amina Hassan na taarifa kamili..

(TAARIFA YA AMINA)

Hii ni kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani WHO, ambalo leo limepitisha azimio jipya lijulikanayo kama "Mfumo wa Malaria Afrika", ambalo lengo lake ni kusaidia nchi wanachama katika kutekeleza vipaumbele maalum ili kutokomeza kabisa malaria Afrika.

WHO inasema ingawa bado safari ni ndefu, visa vya malaria Afrika vimepungua kwa asilimia 66 tangu mwaka 2000. Dr. Frank Lule, mkurugenzi mkuu wa wa kikanda Afrika amesema kilicholeta mafanikio haya Afrika ni..

"Mikakati mitatu ya malaria ni matumizi ya neti zenye dawa, kupulizia dawa ndani ya nyumba, na kudhibiti visa kwa, kuhamishia matibabu mikononi mwa jamii, ambapo kuna uchunguzi wa haraka, ambapo unapanua wigo haraka wa watu kupata matibabu."