Mwanamuziki mwenye ulemavu wa kutoona anga’ra kimataifa
Kuwa mlemavu wa kutoona hakukumzuia kabisa mwanamuziki chipukizi kutoka Nigeria Cobhams Asuquo kushamiri hadi ngazi ya kimataifa.
Hii ni sehemu ya simulizi ya kusisimua katika makala iliyoandaliwa na Joseph Msami ambayo inaangazia juhudi za Shirika la Kimataifa la Haki Miliki WIPO kulinda na kuhifadhi haki za wabunifu, na wenye vipaji mbalimbali wakiwamo waimbaji.