Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNDP yazindua changamoto ya ubunifu kwa vijana kwa ajili ya amani

UNDP yazindua changamoto ya ubunifu kwa vijana kwa ajili ya amani

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo(UNDP) linazindua changamoto ya ubunifu kwa vijana mmojammoja na makundi, ambao watakuwa na mawazo ya ubunifu na kuwashirikisha vijana wenzao katika ujenzi wa amani na kama mawakala wa kuleta mabadiliko Sudan Kusini.

Na kama sehemu ya mchango wa vijana kwa ajili ya amani UNDP itawatunza kwa zawadi ya hadi dola 10,000 washindi. Kimberly Bays ni Afisa wa UNDP Sudan Kusini anaeleza kwa nini wameamua kuzindua mradi huo na wanachokitaka hasa..

(SAUTI YA KIMBERLY)