Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Marimba ya Afrika yameota mizizi Colombia

Marimba ya Afrika yameota mizizi Colombia

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO linapigia chepuo utamaduni wa nyimbo kama sehemu ya kutunza urithi wa dunia katika mila na tamaduni mbali mbali. Muziki unaotumia ala za marimba ambao ni alama ya utamaduni wa watu wenye asili ya Afrika walioko maeneo mbali mbali duniani ikiwemo Ecuador na Colombia ni moja ya vitu ambavyo UNESCO inataka kuhifadhi. Joseph Msami katika makala ifuatayo anasimulia jinsi muziki huo unavyotumika kuhifadhi historia na hadhi ya watu hao wenye asili ya Afrika huko Colombia.