Nchi za Amerika ya Kaskazini na Kati zaahidi kuwalinda wakimbizi
Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR , limekaribisha tamko la San Jose la kuchukua hatua lililotolewa leo, ambapo nchi tisa za Amerika Kaskazini na Kati zimeahidi kuwalinda wakimbizi. Joshua Mmali na taarifa kamili.
(TAARIFA YA JOSHUA MMALI)
Tamko hilo la pamoja ni la kuhakikisha ulinzi kwa wakimbizi kutoka Amerika ya Kati ni hatua kubwa kabla ya mkutano wa Umoja wa Mataifa na Marekani kuhusu wakimbizi na wahamiaji mwezi ujao wa Septemba.
Kamishima mkuu wa wakimbizi Filippo Grandi amesema inaridhisha na kutia moyo sana kuona nchi za Amerika zinakuja pamoja na msimamo wa kikanda wa kubuni suluhisho shirikishi kwa ajili ya watu wanaohitaji msaada wa kuokoa maisha.
Katika taarifa hiyo serikali za Belize, Canada, Costa Rica, El Salvador, Guatemala, Honduras, Mexico, Panama na Marekani, zimeafiki kwamba kuna haja ya kuwalinda kikanda waomba hifadhi, wakimbizi na wakimbizi wa ndani.