Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ziara ya O’Brien Sudan Kusini yamulika mahitaji ya huduma na ulinzi

Ziara ya O’Brien Sudan Kusini yamulika mahitaji ya huduma na ulinzi

Mratibu Mkuu wa masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura, Stephen O’Brien yupo nchini Sudan Kusini kwa kwa ziara ya siku tatu ili kujionea na kutathmini hali ya kibinadamu, na kurejelea wito wa ufadhili.

Mpango wa kibinadamu nchini Sudan Kusini umetoa ombi la dola bilioni 1.3, lakini umepokea asilimia 40 ya fedha zinazohitajika.

Zaidi ya watu milioni moja na nusu ni wakimbizi wa ndani nchini Sudan Kusini, huku watu milioni 4.8 wakiwa hawana uhakika wa kupata chakula. Kumulika zaidi ziara ya Bwana O’Brien, ungana na Joshua Mmali katika makala hii.