Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi wajinoa tayari kushiriki Olimpiki

Wakimbizi wajinoa tayari kushiriki Olimpiki

Siku chache kabla ya michuano ya Olimpiki, timu ya wakimbizi inayoshiriki mashindano hayo katika michezo mbalimbali ikiwemo riadha imewasili mjini Rio Dejenairo tayari kwa kushiriki kwa mara ya kwanza.

Katika Makala ifuatayo Joseph Msami anamulika maandalizi ya wanariadha wakimbizi kutoka nchini Sudan Kusini ambao wamejinoa kambini nchini Kenya.