Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la Wiki: "Kuogopa" na "Kuongopa"

Neno la Wiki: "Kuogopa" na "Kuongopa"

Mchambuzi wako leo ni Nuhu Bakari kutoka CHAKITA, Kenya na anasema "Kuongopea" maana yake ni kudangaya, ndio maana halisi, na anasema mtanzania akikuambia unaniongopea maanake ni unanidanganya, lakini Kenya mtu akikuambia unaniongopea inaweza kuwa na maana nyingine ambayo ni unamuogopa na anasema halitumiki mno kwa sababu ya uoga huo , na katika lugha ya Kiswahili hamna neno kama kuogopea. Kwa hivyo Ongopea maana yake ni "danganya" na Ogopea "tia hofu".