Tanzania iko katika mwelekeo mzuri wa kiuchumi licha ya deni: ADB
Ripoti ya maendeleo ya kiuchumi barani Afrika iliyozinduliwa hapo jana na kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD, imeelezwa kuwa ni muhimu katika kuanza mikakati ya utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu kote duniani.
Wakizungumza mjini Dar es salaam ambapo ripoti hiyo imejadiliwa kwa kuangalia hadhi ya kiuchumi ya Tanzania, wadau wa uchumi wamesema licha ya nchi hiyo kuwa miongoni mwa mataifa yenye mzigo wa madeni, haihatarishi uchumi wake.
Prosper Charles ni mchumi kutoka benki ya maendeleo Afrika ADB.
( SAUTI PROSPER)