Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hofu yatanda kila uchao kwa wapalestina ukingo wa magharibi wa mto Jordan

Hofu yatanda kila uchao kwa wapalestina ukingo wa magharibi wa mto Jordan

Huko ukingo wa magharibi wa mto Jordan, baadhi ya wapalestina wanaishi kwa hofu kubwa kila uchao. Hii ni kutokana na mashambulizi ya kulipiza kisasi yanayofanywa na Israel kutokana na kile inachoeleza kuwa ni mashambulizi yanayofanywa na wapalestina dhidi ya waisraeli. Hali ni zaidi ya kuviziana lakini kama wasemavyo wahenga, vita vya panzi, yaumiayo ni majani. Je ni nani hasa wanaoathiriwa na hali hiyo? Assumpta Massoi anakupeleka huko Mashariki ya Kati kupitia makala hii.