Mpango wa miaka mitano ya kukuza Kiswahili Afrika Mashariki waanzishwa
Wadau mbalimbali wa lugha ya Kiswahili wamekutana hivi karibuni mjini Nairobi, Kenya na kupitisha mpango mkakati wa lugha Kiswahili katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mpango huo wa miaka mitano unanuwia kuimarisha matumizi mapana ya lugha ya Kiswahili kwa kubuni taasisi na asasi za Kiswahili katika nchi za Jumuiya ili kukuza na kueneza lugha hiyo ya kwanza ya kiafrika inayozungumzwa na watu wengi .
Hata hivo katika eneo hilo kumekuwa na changamoto ya viwango vinavyotofautiana vya Kiswahili, Mkakati huo kati ya mambo mengi umechagiza kubadilishana kwa wataalamu na mitaala kama sehemu ya kusawazisha viwango hivyo. Mwandishi wetu wa Maziwa Makuu Ramadhani KIBUGA alihudhuria kongamano hilona ametuandalia makala hii.