Harakati za kulinda watu wenye ualbino
Kwa siku tatu mfululizo kuanzia tarehe 17 mwezi Julai mwaka 2016 nchini Tanzania, kulifanyika mkutano wa ngazi ya juu kuhusu harakati za kulinda watu wenye ulemavu wa ngozi , au ualbino. Lengo la mkutano huo wa kwanza kabisa katika kanda ya Afrika lilikuwa kuleta pamoja viongozi wa serikali, mashirika ya kiraia na watu wenye ualbino ili hatimaye kuibuka na mipango inayotekelezeka mashinani. Je nini kilijiri?
(Makala)