Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Panda miti kwa mazingira bora Uganda

Panda miti kwa mazingira bora Uganda

Wakati athari za mabadiliko ya tabianchi zikionekana dhahiri na kwa kasi, hakuna budi kila mtu kutoa mchango katika kulinda mazingira kwa sasa na kwa kizazi kijacho.

Nchini Uganda, jamii zinahamasishwa katika kupanda miti na wanaoshirikishwa zaidi ni watoto kwani wao ndio waathirika wa uharibifu unaofanyika sasa. John Kibego anatueleza zaidi kuhusu uhamasishaji huo katika makala hii, ungana naye.