Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uharibifu wa vyanzo vya maji unazidi kuchochea uhaba wa bidhaa hii Karagwe, Tanzania

Uharibifu wa vyanzo vya maji unazidi kuchochea uhaba wa bidhaa hii Karagwe, Tanzania

Upatikanaji wa maji katika nchi nyingi barani Afrika unakabiliwa na changamoto nyingi huku mchango wa bindamu na hata mabadiliko ya tabianchi vikiathiri hali hii.

Maji licha ya kwamba ni huduma ya msingi lakini watu wengi hawana uwezo wa kupata bidhaa hii na miongoni mwa sababu ni uharibifu wa vyanzo vya maji. Katika makala hii Tumaini Anatory wa redio washirika Karagwe Fm ya Kagera Tanzania anatupeleka Karagwe kwa ajili ya kupata uelewa kuhusu uhifadhi wa vyanzo vya maji nchini humo, ungana naye.