Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la Wiki- Kandelinya

Neno la Wiki- Kandelinya

Katika Neno la Wiki hii  tunaangazia neno Kandelinya na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, huko nchini Tanzania.

Onni Sigalla anazungumzia matumizi ya neno Kandelinya. Anasema Kandelinya ni birika mahususi kwa ajili ya kutengenezea chai au maji, na pia linaweza kuwa ni birika maalum kwa ajili ya kuoshea mikono kabla na baada ya kula. Kandelinya pia  ni aina ya muhogo ambao ni mchungu na huliwa tu baada ya kuuvundika na kukaushwa kwa ajili ya kutengenezea makopa.