Mahitaji ya wakimbizi na wahamiaji ni kipaumbele chetu: Mwenengabo.
‘‘Tunawasidia wakimbizi na wahamiaji kisaikolojia na kiafya ili kuwapa unafuu wa kimaisha’’ amesema Mkurugenzi wa taasisi ya haki za watu wa asili Afrika Mashariki na kati ECAAIR Fredrick Mwenengabo.
Katika mhojiano na Joseph Msami wa idhaa ya Kiswahili ya redio ya Umoja wa Mataifa Mwenengabo ambaye alihudhuria mkutano wa jamii asilia mjini New York anasema amekutana na wadau wa masuala ya wakimbizi na kibinadamu ili kupata usaidizi zaidi.
Awali anaeleza ujumbe wake katika mkutano uliomalizika wa jamii asilia.
(SAUTIMAHOJIANO)