Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sifuri ama Sufuri, ni lipi?

Sifuri ama Sufuri, ni lipi?

Katika neno la wiki tunachambua neno Sufuri na Sifuri, mchambuzi wetu leo ni, Nuhu Zuberi Bakari ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa Maswala ya Mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA. Maneno haya yote yako kwenye kiswahili lakini ni lipi sahihi kutumia?.

Nuhu Zuberi Bakari anazungumzia matumizi ya maneno haya hususan Kenya na Tanzania.  Anasema Sifuri hutumika Tanzania na Sufuri Kenya, na yote ni sawa, lakini kwa maoni yake anasema Sifuri ndio sahihi zaidi.