Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ajira kwa vijana Afrika ni shida, lazima kuchukua hatua- Mwencha

Ajira kwa vijana Afrika ni shida, lazima kuchukua hatua- Mwencha

Afrika we want! Afrika tuitakayo ndiyo maudhui ya mkutano wa siku moja uliofanyika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ukiwa umebeba mada mbali mbali ikiwemo maendeleo ya kiuchumi na kijamii bila kusahau usawa wa kijinsia. Lakini Afrika yenyewe hadi kuja mbele ya jamii ya kimataifa huku ikiwa tayari imebeba ajenda yake ya 2063 na tayari nchi zimeridhia pia ajenda ya maendeleo endelevu SDGs au ajenda 2030 inataka nini? Assumpta Massoi wa Idhaa hii amezunguzma na Erastus Mwencha, Naibu Mwenyekiti wa kamisheni ya Muungano wa Afrika AU na hapa Bwana Mwencha anaanza kwa kuelezea ujumbe wao.