Baraza Kuu lahitimisha kusikiliza wanaowania wadhifa wa Ban Ki-moon
Ni rais wa Baraza Kuu, Morgens Lykketoft, akifungua vikao vya leo vya Baraza Kuu, katika mchakato wa kihistoria ulio wazi na jumuishi, wa uteuzi wa Katibu Mkuu mpya atakayemrithi Ban Ki-moon, ambaye anahitimisha muhula wake mwishoni mwa mwaka huu. Maneno yake ni yale yale aliyotumia katika vikao vya vya awali Jumanne na Jumatano, akisisitiza utoaji fursa na muda sawa kwa wagombea na wajumbe wa nchi wanachama wanaouliza maswali.
“Mosi, kuhakikisha kuwa uamuzi wa pamoja unawakilisha mtandano imara zaidi wa usalama katika changamoto za sasa. Pili, kwamba Umoja wa Mataifa uliofanyiwa marekebisho unapaswa kuwa kiungo cha kati cha utawala wa kimataifa. Na tatu, kwamba rasilmali zilizopo za Umoja wa Mataifa zinatumiwa vyema zaidi, ili uweze kupata ufanisi wanaotaka wanachama wake na jamii ya kimataifa kwa ujumla.”
“Lakini tunapaswa kujitahidi zaidi, kupitia kushirikiana kwa karibu zaidi, mazungumzo, na kujenga ubia mpana tunavyoweza. Nadhani Umoja wa Mataifa unaweza kupata ufanisi zaidi katika kuhudumia nchi wanachama, na unaweza kuwa mahali bora zaidi pa kufanya kazi. Ni lazima uwe wazi kuhusu unachoweza kufanya na usichoweza kufanya. Ni lazima ushirikiane na nchi wanachama kuona kuwa rasilmali unazopewa zinaelekezwa zaidi panapoweza kupatikana mabadiliko makubwa zaidi”
“Inatoa kipaumbele kwanza kwa ufanyiaji marekebisho usimamizi, kisha maendeleo endelevu na ufadhili kwa ajili ya maendeleo, mfumo wa usalama, haki za binadamu na ushiriki wa raia, uhamiaji, na kisha, jinsi ya kuyatimiza malengo haya. Inamaanisha kuwa tunahitaji vifaa vinavyofaa, ambavyo ni upatanishi, kuendeleza uamuzi wa pamoja, na ubia”
Iwapo hapataibuka wagombea wengine, basi vikao vya leo vitakuwa ndivyo vya mwisho katika mchakato huu unaoendelea wa uteuzi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ambapo kufikia sasa wagombea tisa wamewasilisha hoja zao na kujibu maswali kutoka kwa wajumbe wa nchi wanachama.