Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kumbukizi ya mauaji ya kimbari Rwanda yafanyika kwenye UM

Kumbukizi ya mauaji ya kimbari Rwanda yafanyika kwenye UM

Leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, inafanyika kumbukizi ya mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994. Taarifa zaidi na Amina Hassan.

(Taarifa ya Amina)

Lengo la kumbukizi hiyo ni kuwaenzi watu zaidi ya 800,000 waliouawa miaka 22 iliyopita na kusikiliza ushahidi wa manusura.

Katika muktadha huo, jamii ya Wanyarwanda wanaoishi ughaibuni Marekani walikusanyika hapo jana Jumapili kukumbuka ndugu zao.

Eugenie Mushekimana ni mkurugenzi wa Shirika la Manusura wa Mauaji ya Kimbari..

(Sauti ya Eugenie)

Wengi wa manusura wamesisitiza ujumbe wa maridhiano. Jean-Paul Uwimana ni mmoja wao.

(Sauti ya Jean-Paul