Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mradi wa pamoja waleta nuru vita dhidi ya GBV-Kenya

Mradi wa pamoja waleta nuru vita dhidi ya GBV-Kenya

Nchini Kenya wadau mbali mbali wanashirikiana katika kukabiliana na ukatili wa kijinsia, GBV kupitia programu ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake Jowege.

Programu ya pamoja kati ya Umoja wa Mataifa na serikali ya Kenya. Lengo la programu hiyo ni kuimarisha uwezo wa wahusika ili kuweza kukabiliana na kuzuia ukatili wa kijinsia.

Kulingana na Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu, UNFPA moja ya wadau wanaoendesha miradi mbali mbali nchini Kenya, ukatili wa kijinsia unaweza chukua mfumo wowote ikiwemo, ubakaji, ukatili wa kijinsia au wa kimwili na unaweza lenga mtu wa jinsia yeyote ikiwemo wanaume.

Kenya ni moja ya nchi ambazo zinakabiliwa na tatizo hili. Je ni mikakati ipi ambayo Umoja wa Mataifa na wadau ikiwemo Shirika la Uhamiaji duniani IOM kwa kushirikiana na serikali wamechukua? Basi ungana na Grace Kaneiya katika makala hii.