Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nchini Madagascar, utumwa bado huwakumba watoto

Nchini Madagascar, utumwa bado huwakumba watoto

Bado zaidi ya asilimia 25 ya watoto wenye umri wa kati ya miaka mitano na 17 wanatumikishwa nchini Madagascar, hasa kwenye kazi za nyumbani, limesema Shirika la Kazi duniani ILO.

Tatizo hilo linakumba zaidi maeneo ya vijijini ambapo kwa mujibu wa ILO, asilimia 44 ya watoto wanaotumikishwa hivyo wameajiriwa wakiwa na umri wa kati ya miaka 10 na 12.

ILO imeongeza kwamba mshahara wao wastan ni dola 12 kwa mwezi, ukiwa chini sana ikilinganishwa na mshahara wa chini wa kitaifa ambao ni dola 66 kwa mwezi, wengi wao wakitumikishwa kwa saa zaidi ya 12 kila siku, kinyume na sheria ya kazi ya kitaifa, na wakikosa huduma za msingi za elimu.

Kwa ushirikiano na serikali ya Madagascar ambayo imeunda mpango kazi wa kitaifa mwaka 2004, ILO inafadhili miradi ya kusaidia watoto hawa kuokolewa, kupewa fursa mpya ya kusoma na kuwezesha familia zao kujiendeleza kiuchumi.