Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban akutana na Rais Abbas wa Palestina

Ban akutana na Rais Abbas wa Palestina

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, amekutana na Rais Mahmoud Abbas wa Palestina, ambapo amekariri masikitiko yake makubwa kuhusu ghasia zinazoendelea sasa, na haja ya pande kinzani kuimaliza hali ya utata.

Ban ambaye yupo ziarani Mashariki ya Kati kupigia debe mkutano kimataifa masuala ya kibinadamu mjini Istanbul, mwezi Mei, amesisitiza haja ya kuendeleza hatua za umoja wa Palestina, nay a uongozi wa dhati katika kuijenga upya Gaza.

Aidha, viopngozi hao wawili wamejadili kuhusu mchakato wa amani wa Mashariki ya Kati, ukiwemo mchango wa nchi nne.

Ban amekariri kuwa mazingira mapya ya kisiasa yanapaswa kuwekwa hima kwa ajili ya kurejelewa mazungumzo ya amani kuhusu suluhu la mataifa mawili.