Hakuna lisilowezekana, Libya itafikia mwafaka: Kikwete
Licha ya kwamba taifa limegawanyika kutokana na kuwa na mamlaka nyingi zinaozoongoza, bado kuna matuamaini ya suluhu Libya amesema Mjumbe maalum wa Muungano wa Afrika AU katika mzozo wa Libya Jakaya Kiwete.
Katika mahojiano maalum kwa njia ya simu kutoka Tunisia kulikofanyika mkutano wa kusaka suluhu la kisiasa, Kikwete ambaye pia ni Rais mstaafu wa Tanzania amemueleza Joseph Msami kuwa ameanza hatua za awali za kujifunza kinachotatiza Libya.
( SAUTI MAHOJIANO)