Skip to main content

Bahrain yatakiwa kumwachilia mwanamke mtetezi wa amani

Bahrain yatakiwa kumwachilia mwanamke mtetezi wa amani

Mwakilishi maalumu wa Umoja wa mataifa kuhusu hali ya watetezi wa amani Michel Forst, leo ametoa wito kwa serikali ya Bahrain kumwaachilia mara moja mwanamke mtetezi wa amani na mwanaharakati wa mitandao ya kijamii  Zainab Al-Khawaja, na kumfutia mashitaka yote kwani alikuwa akitekeleza haki yake ya uhuru wa kujieleza.

Bi. Zainab Al-Khawaja  alikamatwa pamoja na mwanae wa miezi 15 mnamo tarehe 14 Machi  kutokana na mashitaka yanayomkabili kwa ajili ya kuchana picha ya mfalme wa Bahrain na kumtusi mfanyakazi wa umma.

Kwa mujibu wa mwakilishi huyo Bi Zainab anashikiliwa kwa mtazamo wake wa kuikosoa serikali.