Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Oman, Umoja wa Mataifa zaandaa mkutano wa baraza linalorasimu katiba Libya

Oman, Umoja wa Mataifa zaandaa mkutano wa baraza linalorasimu katiba Libya

Ufalme wa Oman na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Libya, wametoa mwaliko kwa wanachama wote wa Barza linalorasimu katiba ya Libya (CDA), kwenye mkutano wa mashauriano hapo kesho, kuhusu masuala muhimu ambayo bado hayajatatuliwa. Taarifa zaidi na John Kibego.

(Taarifa ya Kibego)

Rasimu hiyo ya katiba inatazamiwa kutolewa kabla ya kura itakayoamua hatma yake.

Kwenye mkutano wa mashauriano ujumbe wa Umoja wa Mataifa unasaka kusisitiza kanuni ya umiliki wa kitaifa wa katiba ya Libya, ambapo pia watajadili masuala yaliosalia na kuhakikisha kwamba wamekubaliana kuhusu maoni na nyaraka zinazotazamiwa kutolewa.

Ujumbe huo unaamini kuwa, wanachama wote watashirikiana na kuwajibika kwa kuheshimu ibara 30 ya utoaji wa katiba kwa kurasimu katiba inayowakilisha matakwa ya raia wa Libya.