Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Fursa za mafunzo zalenga kuwainua wanawake-Tanzania

Fursa za mafunzo zalenga kuwainua wanawake-Tanzania

Lengo la tano la malengo ya maendeleo endelevu au Ajenda 2030 linaangazia usawa wa kijinsia. Katika kufanikisha lengo hili mikakati muhimu inapaswa kuwekwa ili kuhakikisha kwamba nchi zinafanikiwa. Moja ya mikakati muhimu katika kufanikisha lengo ni kutoa mafunzo kwa wanawake n wanaume ambako nchini Tanzania baadhi ya wanawake wamepata mafunzo yanayolenga kuwainua kiuchumi. Benson Mwakalinga kutoka Redio Washirika Kyela FM ya Mbeya Tanzania amezungumza na baadhi yao, ungana naye katika makala hii.