Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuondoa umaskini kupitia usawa wa kijinsia: Rwanda

Kuondoa umaskini kupitia usawa wa kijinsia: Rwanda

Nchini Rwanda, zaidi ya familia 6,000 wamepatiwa mafunzo ya kuimarisha kipato chao na upatikanaji wa chakula kupitia mifugo.

Kwa mujibu wa Mfuko wa Kimataifa kwa ajili ya maendeleo ya kilimo IFAD ambao umeshirikiana na serikali ya Rwanda katika mradi huo uitwao KWAMP, mafanikio zaidi yamepatikana kwa sababu mradi umehusisha mafunzo kuhusu usawa wa kijinsia.

Tayari Rwanda ikiongoza duniani kwa uwiano wa wanawake bungeni, sasa inategemea kukuza maendeleo kwa kuwapa wanawake nafasi zaidi katika maswala ya kiuchumi.

Kulikoni? Ungana na Joshua Mmali kwenye makala hii...