Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuna matumaini ya watoto wakimbizi kupata elimu licha ya hali ya ukimbizini

Kuna matumaini ya watoto wakimbizi kupata elimu licha ya hali ya ukimbizini

Nchini Ethiopia, idadi ya wakimbizi kutoka Sudan Kusini ni zaidi ya 350,000. Miongoni mwao, Shirika la Umoja wa MAtaifa la Kuhudumia wakimbizi UNCHR linakadiria kwamba zaidi ya 100,000 ni watoto wenye umri wa kwenda shuleni. Lakini nusu yao tu wamejiandikisha shuleni.

Kwenye kambi ya wakimbizi ya Kule ilioko nchini Ethiopia, mvulana mmoja ameshikilia majukumu katika kuwafundishia wenzake.

Ungana na Priscilla Lecomte kwenye makala hii.