Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Umoja wa Mataifa waanza kuondoka Liberia, amani yarejea

Umoja wa Mataifa waanza kuondoka Liberia, amani yarejea

Kuna usemi usemao nyota njema huanza kuonekana asubuhi, usemi huu unaonekana kutimia katika taifa lililoko Afrika Magharibi Liberia,  ambalo baada ya kushuhudia vita ya wenyewe kwa wenyewe taifa hilo sasa linaelekea kwenye nuru.

Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wake nchini humo UNMIL umejiandaa kuondoka nchini humo baada ya kuwezesha ulinzi wa amani hatua iliyoambatana na kusaidia vikosi vya usalama kuimarisha amani nchini humo. Ungana na Joseph Msami katika makala itakayokupa undani zaidi.