Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Radio imetumika sana kupasha habari hususan wakati wa majanga- Mbotela

Radio imetumika sana kupasha habari hususan wakati wa majanga- Mbotela

Umuhimu wa Radio bado ni dhahiri katika mataifa yanaoendelea na hususan wakati wa dharura. Katika ujumbe wa mwaka huu katika kuadhimisha siku ya Radio Duniani ambayo ni Februari 13, Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limesema kwamba radio ina mchango mkubwa wakati wa kukabiliana na majanga.

Katika mahojiano yafuatayo kutoka Kenya Geoffrey Onditi wa radio mojawapo ya washirika wetu, KBC, amezungumza na mtangazaji gwiji Leonard Mambo Mbotela, mwenye umaarufu unaovuka mipaka ya Kenya, akimweleza umuhimu wa chombo hiki adhimu.