Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP yafikisha misaada Yemen

WFP yafikisha misaada Yemen

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP limefanikiwa kufikisha misaada ya chakula kwenye maeneo yaliyozingirwa mjini Taiz nchini Yemen ambapo watu wanakumbwa na njaa.

Kwa mujibu wa taarifa ya WFP iliyotolewa leo, msafara wa WFP umepeleka vyakula vya mwezi mmoja kwa familia 3,000 baada ya kutimiza mazungumzo na pande kinzani za mzozo kuhusu umuhimu wa kuruhusu misaada ya kibinadamu,

WFP imeongeza kwamba mjini Taiz, maisha ya familia moja kati ya tano yako hatarini kwa sababu ya utapiamlo.

Kwa ujumla, watu milioni 7.6 nchini Yemen wanakumbwa na njaa.