Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wananchi wa Sudan Kusini wamechoka kuwa tegemezi- Mogae

Wananchi wa Sudan Kusini wamechoka kuwa tegemezi- Mogae

Hivi karibuni, Festus Mogae ambaye ni mwenyekiti wa kamisheni ya pamoja ya kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa makubaliano ya amani nchini Sudan Kusini, JMEC, alikuwa ziarani kwenye maeneo ya Malakal na Bentiu. Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kumwezesha kukutana na pande mbali mbali ikiwemo serikali, pande kinzani na hata mashirika yanayotoa misaada ya kibinadamu. Ziara ya Mogae ambaye pia ni rais wa zamani wa Botswana, ilianzia Malakal na hatimaye Bentiu, je alishuhudia nini? Grace Kaneiya anafafanua kwenye makala hii.