Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kongamano la WIPO lakutanisha wabunifu wa mitindo Afrika kuhusu hati miliki

Kongamano la WIPO lakutanisha wabunifu wa mitindo Afrika kuhusu hati miliki

Sekta ya ubunifu wa mitindo barani Afrika ina uwezo mkubwa wa kukua, kwani kuna wingi wa talanta na ubunifu kote barani. Kulingana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hati Miliki Duniani, WIPO, matumizi yafaayo ya hati miliki yanaweza kuchangia maendeleo endelevu ya sekta hiyo. Kwa mantiki hiyo, hivi karibuni, WIPO iliandaa kongamano kuhusu hati miliki kwa bara la Afrika linaloibuka, mjini Dakar, Senegal, ambako pia kulifanyika maonyesho ya sanaa na mitindo, kama anavyosimulia Joshua Mmali katika Makala hii.