Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Bora baridi kuliko mashambulizi huko Syria; wasema wakimbizi

Bora baridi kuliko mashambulizi huko Syria; wasema wakimbizi

Mzozo wa Syria ukiwa umeingia mwaka wa tano, wakimbizi waliosaka hifadhi kwenye bonde la Bekaa nchini Lebanon wanahaha kujinusuru na baridi kali. Theluji ya kwanza imeanguka na maelfu ya wakimbizi ambao tayari wamekumbwa na machungu, wanazidi kuhaha, na miongoni mwao ni Abu Hamada.

Yeye, mkewe na watoto wao 10 waliwasili Bekaa miaka miwili iliyopita na sasa wanahaka kuhakikisha kuwa wanapata joto la kutosha ili kunusuru familia yao. Vifaa vya kutoa joto, mafuta na makazi ni usaidizi wa Umoja wa Mataifa na wadau wake wa misaada lakini bado hali si shwari.

Assumpta Massoi anafafanua zaidi kwenye makala hii.