Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Muarobaini wa kutokomeza kipindupindu ni usafi: Dk Azma

Muarobaini wa kutokomeza kipindupindu ni usafi: Dk Azma

Mlipuko wa ugonjwa kipindupindu ulioanza Agosti 15 mwaka huu nchini Tanzania unaendelea kugharimu mamia ya maisha ya watu kwani ugonjwa huo sasa umesambaa katika mikoa 21 ya taifa hilo la Afrika Mashariki.

Hata hivyo wadau wa afya wakiratibiwa na shirika la afya ulimwenguni WHO na mamlaka za afya za serikali wanahaha kunusuru maisha zaidi kwa mikakati ya kutoa elimu kwa uma. Dk Azma Simba kutoka wizara ya afya, ambaye ni mtaalamu wa afya ya jamii katika fani ya epidemiolojia amemweleza Joseph Msami wa idhaa hii katika mahojiano maalum hali ya kipindupindu ilivyo.

(MAHOJIANO)