UM wapigia chepuo ushiriki wa wanawake katika vyombo vya usalama Somalia
Nchini Somalia taifa ambalo limekuwa katika mizozo kwa takribani miongo miwili, ujenzi wake unaimarika katika nyanja tofauti ikiwamo ushirikishwaji wa wanawake katika vyombo vya usalama.
Umoja wa Mataifa na wadau wengine kwa kutambu ahilo unasaidia juhudi hizo za taifa hilo liliko katika pembe ya Afrika, wameendesha mafunzo kuhusu ushirikishwaji na ushiriki wa wanawake hususani askari. Ungana na Joseph Msami katika makala ifuatayo.