Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watoto Zanzibar wajiamini zaidi kupitia sheria mpya ya watoto

Watoto Zanzibar wajiamini zaidi kupitia sheria mpya ya watoto

Sheria ya Watoto ya Zanzibar ya mwaka 2011 hivi karibuni imeshinda tuzo ya sera za mustakabali yaani Future Policies, miongoni mwa sheria 19 zilizowania tuzo hiyo. Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF nchini Tanzania, sheria hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa katika kupazia sauti ya watoto na kupambana na vitendo vya ukatili dhidi yao. Kulikoni? Ungana na Priscilla Lecomte kwenye makala hii.