Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ujasiri wa wanawake ndiyo hunipa ujasiri: Dk Mukwege

Ujasiri wa wanawake ndiyo hunipa ujasiri: Dk Mukwege

Jana katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa mara ya kwanza kumeonyeshwa filamu iitwayo  mwanaume anayerekebisha wanawake ikiwa inamulika maisha ya Dk Denis Mukwege anayesaidia maelfu ya wanawake waliothiriwa kutokana na ubakaji nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya kongo DRC.

Dk Mukwege ambaye ni mshindi wa tuzo ya Sakharov kutoka Muungano wa Ulaya anayetoa tiba katika mazingira magumu  ya machafuko katika hospitlai iitwayo  Panzi iliyoko Bukavu DRC,  ameiambia idhaa hii muda mfupi baada  ya filamu hiyo kile kinachompa hamasa kuendelea na kazi hiyo ngumu.

(SAUTI DK MUKWEGE)   

Mahojiano kamili na Dk Mukwege pamoja na undani wa filamu hiyo yatakujia katika matangazo yetu yajayo.